Maagizo ya Kutuma Kazi

Tafadhali tuma nakala au kitabu (ngano, ushairi na wasifu, mkusanyiko wa hadithi fupiau, riwaya) iliyochapishwa katika miaka miwiki kabla mwaka wa tuzo kwa: kiswahiliprize@cornell.edu kabla ya Agosti, 5, 2019.

Mwandishi moja anaweza kutuma kazi moja pekee yake kila mwaka.

  • Nakala hazifai kuwa chini ya maneno 50,000 kwa ngano na kurasa 60 kwa ushairi
  • Kazi zote lazima ziwe katika Kiswahili
  • Kazi zinafaa kutumwa kama faili ya Microsoft Word au Rich Text. Mada ya hadithi iwe jina la faili.
  • Kurasa ya kwanza ya hadithi iwe na kichwa cha hadithi na hesabu ya maneno.
  • Kazi ichapishwe kwa mtindo wa Times New Roman, ukubwa wa pointi 12 na nafasi kati ya mistari ya 1.5.
  • Kazi zitumwe kama mwambatano wa barua pepe.
  • Barua pepe inafaa kuwa na habari ifuatayo: Jina rasmi, Lakabu ya kuandika, Nambari ya simu, Tawasifu Fupi, Umri na Nchi ya Makazi
  • Kwa kazi zilizochapishwa, tafadhali mwelekeze mchapishaji wako atume nakala tatu kwa Idara ya Masomo na Utafiti ya Afrikana (Africana Studies and Research Center, 310 Triphammer Road, Ithaca, NY 14850)
Skip to toolbar